Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki (Kiing. East African Rift Valley) ni maumbile ya kijiolojia yanayoanza katika Mashariki ya Kati na kuendelea hadi Msumbiji. Ni kati ya maajabu makubwa ya dunia. Ufa huu ulitengenezwa miaka milioni 25 iliyopita kutokana na mwendo wa mabamba ya gandunia ya Afrika na Uarabuni.[1] Mwendo huu umesababisha pia farakano ndani ya bamba la Afrika na wataalamu huamini kuwa Afrika ya Mashariki iko katika mwendo wa kuachana na Afrika kwa jumla.[2]