Hammurabi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Hammurabi (takr. 1810 KK - 1750 KK) alikuwa mfalme wa sita wa mji wa Babeli akapanua eneo lake na kuunda milki ya kwanza ya Babeli. Anajulikana hasa kwa mkusanyo wa sheria za Hammurabi ambazo ni kati ya sheria za kwanza za dunia zilizoandikwa.
Hammurabi alirithi ufalme kutoka kwa baba yake akitawala eneo la mji wa Babeli kama dola-mji tu. Katika miaka ya utawala wake alifaulu kupanua himaya yake hadi kutawala Mesopotamia yote. Hivyo alianzisha milki ya kwanza ya Babeli.