Johann Wolfgang von Goethe
From Wikipedia, the free encyclopedia
Johann Wolfgang von Goethe alikuwa mwandishi, mshairi, mwanasiasa, mwanafalsafa na mwanasayansi Mjerumani anayekumbukwa kama mwandishi mkuu katika fasihi ya Ujerumani.
Alizaliwa mjini Frankfurt am Main tar. 28 Agosti 1749 akafa Weimar 22 Machi 1832. Alisoma sheria lakini alianza kuandika riwaya za kwanza akiwa mwanafunzi.