Makinikia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Makinikia (Kiing. ore concentrate) ni jina la mchanganyiko wa madini, miamba na wakati mwingine kemikali ambao hutokana na shughuli za uchimbaji wa metali. Metali nyingi kama chuma, shaba au dhahabu hazipatikani kwa umbo safi lakini kama mtapo (ore) ndani ya miamba inayochimbwa. Mtapo unaopatikana ardhini huwa na asilimia kubwa ya miamba ambayo haina tija kiuchumi. Hivyo mtapo hupelekwa kwa kifaa cha kuponda ambapo sehemu yenye madini husika inatenganisha na sehemu isiyo na madini. Mbinu zinazotumiwa kutenganisha sehemu hizi ni pamoja na kutumia nguvu ya sumaku, graviti au kemikali. Matokeo yake ni makinikia ambamo kiwango cha metali ni kubwa kuliko katika mtapo uliochimbwa.
Makinikia inapelekwa hadi kiwanda ambako madini yake hutenganishwa zaidi na kusafishwa.