Mbawavijiko
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mbawavijiko ni wadudu wadogo hadi wakubwa kiasi wa familia Nemopteridae katika familia ya juu Myrmeleontoidea wa oda Neuroptera walio na mabawa marefu na membamba ya nyuma. Mabawa hayo ya mbawavijiko wa kweli ni pana zaidi mwishoni na yanafanana na vijiko vyenye mashikio marefu. Spishi za nusufamilia Crocinae huitwa mbawanyuzi, kwa sababu mabawa ya nyuma hayana sehemu pana. Familia hii ina spishi chini ya 200, ambazo hutokea kanda za kitropiki na kinusutropiki duniani kote, isipokuwa Amerika ya Kaskazini, katika maeneno makavu hasa.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Mbawavijiko | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Nemoptera bipennis | ||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
| ||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||
Nusufamilia 2, jenasi 5:
| ||||||||||||||||
Funga