Mlango wa mashua
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mlango wa mashua (Kiing. lock) ni kifaa kinachoruhusu kupandisha au kushusha mashua, boti au meli kati ya mito na mifereji yenye usawa tofauti wa maji. Sehemu kuu ya mlango wa mashua ni chemba cha maji ambacho wa kawaida huwa na geti mbili; moja upande wa usawa wa juu wa maji na nyingine upande wa usawa wa chini wa maji.Chumba huwa na urefu unarohusu mashua au meli kuingia wakati geti zote zinafungwa.