Symphony No. 5 (Beethoven)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Symphony No. 5 in C minor, Op. 67 ni simfoni iliyotungwa na mtunzi wa Opera kutoka nchini Ujerumani, Ludwig van Beethoven. Hii ni simfoni ya 5 katika simfoni zake tisa. Ilitungwa kati ya 1804 na 1808. Hii ni moja kati ya simfoni maarufu zaidi katika kazi za muziki wa classical.
Simfoni ina miendo au mitindo minne: ya kufungulia sonata allegro, ya polepole andante, ya haraka scherzo ambayo hii inaongoza hadi mwisho wa simfoni.
Kwa mara ya kwanza simfoni hii ilitumbuizwa mjini Vienna katika tamasha lililofanyika katika ukumbi wa Theater an der Wien mnamo 1808. Simfoni yake Namba Sita nayo pia ilitumbuizwa kwa mara ya kwanza katika tamasha hilo. Tangu hapo Simfoni Na. 5 ikawa moja kati ya kazi za muziki wa classical unaojulikana kupita maelezo.