Angakaskazi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Angakaskazi (anga ya kaskazini, kwa Kiingereza "northern sky") ni sehemu za anga zinazoonekana kwa mtazamaji kwenye nusutufe ya kaskazini ya Dunia yetu. Ufafanuzi wake ni "sehemu ya anga upande wa kaskazini wa ikweta ya anga".
Iko kinyume cha angakusi.