![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/fa/Flag_of_the_People%2527s_Republic_of_China.svg/langsw-640px-Flag_of_the_People%2527s_Republic_of_China.svg.png&w=640&q=50)
Bendera ya China
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bendera ya Jamhuri ya Watu wa China ilionyeshwa rasmi mara ya kwanza tar. 1 Oktoba 1949 baada ya ushindi wa Wakomunisti juu ya Kuomintang katika vita ya wenyewe kwa wenyewe ya China.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/fa/Flag_of_the_People%27s_Republic_of_China.svg/640px-Flag_of_the_People%27s_Republic_of_China.svg.png)
Bendera ni nyekundu ikionesha nyota tano za dhahabu. Nyota kubwa inamaanisha utawala wa chama cha kikomunisti.
Nyota nne ndogo ni za tabaka nne zilizotakiwa kubeba mapinduzi:
- wafanyakazi
- wakulima
- raia wa kawaida
- mabepari wenye nia ya kujenga taifa