From Wikipedia, the free encyclopedia
Bendera ya Nigeria ina milia ya kusimama mitatu, miwili ya nje ni kijani na ile ya katikati ni nyeupe.
Bendera ilipatikana katika mashindano ya kitaifa kabla ya uhuru mwaka 1959 na kuonekana rasmi mara ya kwanza tarehe 1.10.1960. Mshindi aliyetunga bendera hii alikuwa mwanafunzi wa uhandisi Michael Taiwo Akinkunmi kutoka Ibadan.
Rangi ya kijani inatakiwa kuonyesha misitu na mashamba yenye rutuba na mlia mweupe humaanisha amani.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.