Beseni la Columbia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Beseni la Columbia (kwa Kiingereza: Columbia Plateau au Columbia Basin) ni eneo maalum la kijiolojia na kijiografia kaskazini-magharibi mwa Marekani, likiwa katika majimbo ya Marekani ya Washington, Oregon, na Idaho. Ni eneo kubwa lililotokana na mkondo wa mwamba wa gumawesi (basalt) ulioenea kati ya milima ya Cascades na Milima ya Rocky Mountains katika kipindi cha milipuko ya volkeno iliyopandisha magma kutoka koti la Dunia ambayo iliganda kwenye uso wa ardhi. Mto Columbia unatiririka katika eneo hilo.