![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/0a/Vladimirskaya.jpg/640px-Vladimirskaya.jpg&w=640&q=50)
Ubikira wa kudumu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ubikira wa kudumu ni sifa ambayo Bikira Maria anapewa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki, pamoja na Waprotestanti wachache, akiwemo Martin Luther. Ni imani yao[2][3][4][5][6][7] kuwa Mama wa Yesu anastahili kuitwa “Bikira daima” (kwa Kigiriki ἀειπάρθενος, aeiparthenos; kwa Kilatini sempervirgo) kwa sababu alimchukua mimba akiwa bikira, akamzaa bila ya kupotewa na ubikira, akabaki bikira hadi mwisho wa maisha yake.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/0a/Vladimirskaya.jpg/320px-Vladimirskaya.jpg)
Imani hiyo inajitokeza katika maandishi ya Mababu wa Kanisa wa karne ya 4, halafu katika matamko ya mitaguso mikuu.