Kerala
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kerala (Malayalam: കേരളം, Kēraḷam) ni jimbo ya Uhindi lililopo kwenye kusini magharibi ya nchi hii. Mji mkuu wake ni Thiruvananthapuram.
Kerala ina eneo la 38,863 km² na wakazi 33,268,000 (2008). Msongamano wa watu ni 856 kwa km². Jimbo hili lilipata mipaka yake mwaka 1956 kufuatana na maeneo yanayokaliwa na wasemaji wa Kimalayalam. Jina la jombo latokana na neno kwa minazi "kera".
Kerala ni jimbo lenye asilimia kubwa ya Wakristo kati ya majimbo yote ya Uhindi. Inaaminiwa ya kwamba asilimia kubwa ya Wakristo (20%) na Waislamu (24 %) imetokana na historia ndefu ya biashara na nchi za Mashariki ya Kati na pia Afrika ya Mashariki ya kwamba walikuwa wafanyabiashara walioleta imani zao hapa. hata hivyo kidogo zaidi ya nusu ya wakazi ni Wahindu.