Lugha za Kiberberi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kiberberi au Kiamazighi ni jina la kundi la lugha zinazosemwa hasa Moroko na Aljeria lakini pia kati ya wakazi wa jangwa kubwa la Sahara hadi eneo la Sahel. Ni lugha ya Waberberi wanaoishi kati ya wasemaji wa Kiarabu katika Afrika ya Kaskazini.
Aina za Tamazight au lugha za Kiberber katika Afrika ya Mashariki. | |
Kitwareg | Kizayani |
Kirifi | Kishanawa |
Kikabile | Kishawia |
Kishilha | Kiberberi ya Sahara |
Kiberberi ni kati ya lugha za Kiafrika-Kiasia. Wasemaji wa Kiberberi watazamiwa kuwa wenyeji asilia wa Afrika ya Kaskazini kabla ya kuja kwa Waroma wa Kale au kwa Waarabu.
Tangu uenezaji wa Kiarabu matumizi ya Kiberberi kimerudi nyuma polepole. Wakazi wengi wa nchi za Afrika ya Kaskazini ni wa asili ya Kiberber lakini kwa kawaida kupotea kwa lugha humaanisha pia upotevu wa tabia ya kuwa Berber. Leo hii wamebaki wasemaji milioni 10 na wengi wao hutumia lugha yao pamoja na Kiarabu au Kifaransa katika maisha ya kila siku.