![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/44/Aert_de_Gelder_004.jpg/640px-Aert_de_Gelder_004.jpg&w=640&q=50)
Kitabu cha Esta
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kitabu cha Esta (jina lake huandikwa pia Ester na "Esther") ni kitabu cha Biblia ya Kiebrania, na hivyo pia cha Agano la Kale, ambalo ni sehemu ya kwanza ya Biblia ya Kikristo. Kiliandikwa kwanza kwa Kiebrania.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a5/Esther_Megillah_Italy_1616.jpg/640px-Esther_Megillah_Italy_1616.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/44/Aert_de_Gelder_004.jpg/640px-Aert_de_Gelder_004.jpg)
Tafsiri ya kitabu cha Esta inavyopatikana katika Septuaginta imeongezewa sana; nyongeza hizo za Kigiriki zinahesabiwa na Kanisa Katoliki na wengineo kuwa sehemu za kitabu yenye uvuvio wa Roho Mtakatifu ingawa si sehemu za hadithi asili. Ni katika nyongeza hizo tu kwamba Mungu anatajwa na mtazamo wa imani unajitokeza.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.