Mohandas Karamchand Gandhi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mohandas Karamchand Gandhi (kwa Kigujarati: મોહનદાસ કરમચંદ ગાંધી; 2 Oktoba 1869 - 30 Januari 1948), maarufu zaidi kwa jina la Mahatma Gandhi, alikuwa mwanasheria, mwanafalsafa, mwanaharakati wa haki za binadamu na kiongozi wa siasa nchini Uhindi.
Anajulikana hasa kama kiongozi wa harakati za uhuru wa Uhindi aliyepinga na kushinda ukoloni kwa njia ya amani bila ya matumizi wa mabavu au silaha.