![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/4a/Mass_demonstration_in_Iran%252C_date_unknown.jpg/640px-Mass_demonstration_in_Iran%252C_date_unknown.jpg&w=640&q=50)
Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yalitokea katika mwaka 1979 nchini Uajemi (Iran) (mwaka 1357 katika kalenda ya Kiajemi). Yalimaliza utawala wa kifalme wa Shah Mohamed Reza Pahlavi na kuleta dola jipya la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/4/4a/Mass_demonstration_in_Iran%2C_date_unknown.jpg/640px-Mass_demonstration_in_Iran%2C_date_unknown.jpg)
Kiongozi mpya wa nchi alikuwa Ayatollah Ruhollah Khomeini, aliyerudi Iran katika Februari 1979 na kuwa kiongozi aliyekubaliwa na wananchi wengi. Katika kipindi cha miezi michache tangu kurudi kwake utawala wa Shah uliporomoka, viongozi wa awali waliuawa, kukamatwa au kukimbia nchi. Mwisho wa mwezi wa Machi 1979 wananchi wengi walipiga kura na kuchagua "Jamhuri ya Kiislamu" kama dola jipya. Katika mwezi wa Desemba katiba mpya ya Jamhuri ya Kiislamu ilikubaliwa katika kura ya wananchi.