From Wikipedia, the free encyclopedia
Mlango wa mashua (Kiing. lock) ni kifaa kinachoruhusu kupandisha au kushusha mashua, boti au meli kati ya mito na mifereji yenye usawa tofauti wa maji. Sehemu kuu ya mlango wa mashua ni chemba cha maji ambacho wa kawaida huwa na geti mbili; moja upande wa usawa wa juu wa maji na nyingine upande wa usawa wa chini wa maji.Chumba huwa na urefu unarohusu mashua au meli kuingia wakati geti zote zinafungwa.
Milango ya mashua inahitajika
Usawa wa maji ndani ya chemba hubadilishwa hadi inalingana na upande ambao mashua inaelekea. Mabadiliko hayo hutekelezwa ama kwa kufungua geti upande wa maji juu na hivyo chemba chote kinajaa sawa na usawa wa juu. Hapa mashua kutoka upande wa juu inaweza kuingia na geti ya juu inafungwa.
Sasa geti ya chini inafunguliwa kidogo na maji hutoka hadi kufikia usawa wa upande wa chini. Mara usawa huo wa chini umefikiwa, geti ya pili inafunguliwa kabisa na mashua inaweza kuondoka upande wa usawa chini.
Wakati mashua inahitaji kupanda, maji ndani ya chemba inatolewa kwa kufungua geti upande wa chini. Mara usawa ndani ya chemba unalingana na sehemu ya chini, mashua inaingia na geti inafungwa. Sasa maji huingizwa kutoka upande wa juu na chemba kinajaa maji hadi kufikia usawa wa juu. Sasa geti ya juu inafunguliwa na mashua inaweza kuendelea upande wa juu.
Mifereji wakati mwngine huwa na mfululizo wa milango inayofuatana kama sehemu za ngazi. Zinapatikana hasa kwenye milango ya zamani iliyoendeshwa kwa nguvu ya mkono.
Siku hizi milango ya kisasa huendeshwa kwa nguvu ya mashine ina uwezo wa kushusha maji ndani ya chemba kimoja mita nyingi zaidi.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.