Msikiti wa Sultan Ahmed
From Wikipedia, the free encyclopedia
Msikiti wa Sultan Ahmed ni msikiti mashuhuri mjini Istanbul katika nchi ya Uturuki. Inajulikana pia kwa jina la "msikiti buluu" kutokana na rangi ya vigae vinavyopamba undani wake.
Msikiti huu ulijengwa kuanzia mwaka 1609 - 1616 kwa maagizo ya Sultani Ahmed I aliyetawala milki ya Osmani.
Ni msikiti mkuu wa Istanbul ukihesabiwa kati ya majengo mazuri na muhimu ya usanifu wa Kiosmani.