Mtakatifu Paulo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtume Paulo (7-67 hivi) ni mmisionari mkuu wa Yesu Kristo katika historia ya Kanisa.
Alitangaza kifo na ufufuko wake katika nchi karibu zote zilizopo kaskazini kwa Bahari ya Kati.
Alimaliza ushuhuda wake kwa Yesu kwa kufia dini yake mjini Roma wakati wa dhuluma iliyoanzishwa na Kaisari Nero.
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Sherehe yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 29 Juni pamoja na ya Mtume Petro, lakini pia uongofu wake una sikukuu maalumu, tarehe 25 Januari[1].