Pilau
From Wikipedia, the free encyclopedia
Pilau (pia: pilao; kwa Kiingereza hujulikana kama pilaf; kwa lugha nyingine kama Kiajemi, Kiazeri, Kikazakh, Kikyrgyz, Kituruki, Kiuzbeki, Kiturkmeni, Kiurdu, Kihindi, Kipashto n.k.: polo, polao, pilaf, pilav, pilaff, plov au pulao; maneno haya yote yanatoka katika lugha ya Kiajemi پلو, ambalo katika Kiajemi ya Kiirani linatamkwa: Polow), ni mlo ambao nafaka, kama vile mchele au ngano uliopasuliwa, hubadilishwa rangi kuwa hudhurungi katika mafuta, na kisha hupikwa katika supu ambayo ina ladha.
Kutegemeana na vyakula vya eneo husika, pilau inaweza kujumuisha aina mbalimbali za nyama na mboga. Pilau na milo sawa nayo ni maarufu katika vyakula vya Mashariki ya Kati, Asia ya Kati na Asia ya Kusini, Afrika ya Mashariki, Amerika ya Kilatini, na Karibi.