Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1992
From Wikipedia, the free encyclopedia
Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1992 ulikuwa wa 52 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 3 Novemba. Upande wa "Democratic Party", mgombea Bill Clinton (pamoja na kaimu wake Al Gore) aliwashinda mgombea wa "Republican Party", Rais George H. Bush (pamoja na kaimu wake Dan Quayle), na mgombea Ross Perot.