Canberra

From Wikipedia, the free encyclopedia

Canberra
Remove ads

Canberra ni mji mkuu wa Australia mwenye wakazi 330,000. Si sehemu ya jimbo lolote la shirikisho la Australia lakini limepewa eneo lake la kitaifa kando la mto Molonglo ndani ya eneo la jimbo New South Wales.

Thumb
Ramani ya Canberra
Ukweli wa haraka Habari za kimsingi, Mahali ...

Iko kilomita 300 kusini magharibi ya Sydney na kilomita 650 kaskazini-masahriki ya Melbourne.

Remove ads

Mji wa kupangwa

Canberra ni mji mpya uliopangwa na ujenzi ukaanza mwaka 1913. Msanifu Mwamerika Walter Burley Griffin alipanga ramani ya mji mwenye bustani nyingi na barabara zilizufuata mpangilio wa duara, pembetatu na miraba.

Alianza kwa kuchukua mto Molongolo kama mhimili wa maji unaokatwa na mhimili wa kwanza kwenye nchi ni uwazi kati ya nyumba ya bunge na makumbusho kwa ajili ya marehemu wa vita.

Mistari mingine muhimu ni "pembetatu ya bunge" kwa barabara tatu pana na nyofu kati ya kilima cha bunge, kilima penye kitovu cha mji mwenyewe na kilima penye wizara ya jeshi. Mikono miwili ya pembetatu inayotoka bungeni inavuka mto kwa madaraja.

Remove ads

Historia

Kabla ya kuundwa kwa Canberra miji ya Sydney na Melbourne ilishindana juu ya nafasi ya mji mkuu. 1908 azimio la kujenga mji mpya likafanywa mahali kati ya miji miwili mikubwa.

Neno "Canberra" lina asili katika lugha ya [Aborigini|Maaborigini]] walio wenyeji asilia wa Australia. Maana yake ni "mahali pa mkutano".

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads