Dado

From Wikipedia, the free encyclopedia

Dado
Remove ads

Dado (pia: Audoin, Audoen, Owen na Ouen wa Rouen; Sancy, Ufaransa, 609Clichy, Ufaransa, 686)[1][2][3] alikuwa waziri wa Wafaranki na halafu askofu.

Thumb
Sanamu ya Mt. Audoin (kushoto) na Mt. Waninge (kulia), huko Fécamp, Ufaransa.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 24 Agosti[4].

Maisha

Mtoto wa mtakatifu Authaire (Audecharius), alilelewa katika ikulu ya mfalme Chlothar II (aliyefariki 629), ambapo alipata elimu na uanajeshi pamoja na vijana wengine wa koo maarufu.

Baadaye alisimamia mali ya Dagobati I[5], akishika sana maadili[6] na akiwa na marafiki kama watakatifu Wandrili, Didier wa Cahors na Eligius wa Noyon, ambaye Dado aliandika habari za maisha yake.

Mwaka 635 pamoja na ndugu zake Ado na Rado alianzisha abasia ya Rebais, halafu monasteri ya Mt. Wandrili huko Rouen, na nyingine ya kike huko Fécamp.

Mwaka 641 alifanywa askofu wa Rouen, jimbo aliloliongoza vizuri kwa miaka 43, akijenga makanisa na monasteri.[5][7]

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads