Forum for the Restauration of Democracy

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Forum for the Restauration of Democracy (FORD) ilikuwa kwanza harakati halafu chama cha kisiasa nchini Kenya.

Chanzo 1991

Ilianzishwa mwaka 1991 na wanasiasa waliopinga mfumo wa chama kimoja na utawala wa KANU chini ya rais Daniel arap Moi. Shabaha ilikuwa mabadiliko ya kuruhusu vyama vingi na uhuru wa kidemokrasia. Wakati ule chama cha pekee kilichoruhusiwa kilikuwa KANU. Mfumo wa chama kimoja uliporomoka katika nchi nyingi za dunia baada ya mwisho wa ukomunisti na mabadiliko yaliyokwenda sambamba na mwisho wa vita baridi katika Afrika.

Remove ads

Waanzilishi

Kati ya waanzilishaji walikuwa Jaramogi Oginga Odinga, Kenneth Matiba, Martin Shikuku, Masinde Muliro na Michael Wamalwa. Mwanzoni FORD ilipigwa marufuku lakini baadaye Moi alilazimishwa na nchi za nje walisaidia sehemu kubwa ya mapato ya serikali kukubali kuwepo kwa FORD.

Mwaka 1992 KANU ilikuwa tayari kubadilisha katiba ya kuruhusu vyama vingi. Walioanzisha vyama mara moja walikuwa Odinga aliyeandikisha FORD kama chama na Mwai Kibai aliyeandikisha Democratic Party (DP). FORD ilikuwa mwanzoni chama cha upinzani wa kitaifa wakati DP ilikuwa na nguvu katika maeneo ya Wakikuyu hasa.

Remove ads

Farakano 1992 juu ya uongozi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads