Hamad bin Thuwain wa Zanzibar

Sultani wa Zanzibar From Wikipedia, the free encyclopedia

Hamad bin Thuwain wa Zanzibar
Remove ads

Sayyid Hamad bin Thuwain Al-Buwsaid (kwa Kiarabu: حمد بن ثويني البوسعيد‎; 185725 Agosti 1896) alikuwa Sultani wa tano wa Zanzibar. Alitawala Zanzibar kuanzia tarehe 5 Machi 1893 hadi 25 Agosti 1896.

Thumb
Sultani Hamad Bin Thuwain, 1890

Maisha

Sayyid Hamad bin Thuwaini Al-Busaid anadaiwa alizaliwa katika kisiwa cha Zanzibar mnamo mwaka 1857. Alimuoa binamu yake, Sayyida Turkia bint Turki, ambaye alikuwa binti ya Turki bin Said, Sultani wa Muscat na Oman.

Sayyid Hamad bin Thuwaini Al-Busaid alifariki ghafla tarehe 25 Agosti 1896 saa 5:40 asubuhi, ikisemekana mara baada ya kupewa sumu na binamu yake Khalid bin Barghash, ambaye alijitangaza kuwa sultani mpya. Khalid aliendelea kushikilia kiti cha enzi kwa siku tatu tu kabla ya kuondolewa na majeshi ya Waingereza katika vita vya Uingereza dhidi ya Zanzibar, vinavyotambulika kama vita vya muda mfupi kabisa katika historia.[1].

Remove ads

Medali za Heshima

  • Italia: Grand Cross of the Order of the Crown of Italy (1893)
  • Britania: Knight Grand Commander of the Order of the Star of India (1894)
  • Ujerumani: Grand Cross of the Order of the Red Eagle, 1st Class (1895)

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads