Joyce Cherono Laboso

Mwanasiasa wa Kenya (1960-2019) From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Dk. Joyce Cherono Laboso ni mwanasiasa wa Kenya na mbunge katika bunge la Kenya

Eneo Bunge

Yeye anawakilisha Jimbo la uchaguzi la Sotik katika bunge la Kumi. Alikichukua kiti hiki kutoka kwa dadake Lorna Laboso ambaye alifariki katika ajali ya ndege mnamo 10 Juni 2008.

Matokeo ya Uchaguzi Mdogo

Katika Uchaguzi mdogo uliofanyika 25 Septemba 2008, Dk. Laboso aliyekuwa akiwania kiti hicho kwa tiketi ya ODM, aliwabwaga wapinzani wengine 11 na kujinyakulia kura 23,880; ushindi wa zaidi ya kura 10,000 kuliko mpinzani wake wa karibu Alexander Sitienei aliyezoa kura 13,843.

Taaluma nyingine

Kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge, Dk. Laboso alikuwa mkufunzi wa lugha ya Kifaransa katika Chuo Kikuu cha Egerton.

Sasa hivi ni mwanakamati katika Kamati ya Kitaifa ya Jinsia na Maendeleo.

Tazama Pia

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads