Klabu ya mbwa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Klabu ya mbwa (kutoka Kiingereza: kennel club) mara nyingi huwa ni mkusanyiko wa wafugaji wa mbwa, wakijadili mambo yanayohusu uzalishaji wa mbwa. Vilianza kuwa maarufu katikati ya miaka ya 1800. Klabu hizi hudumisha viwango vya uzalishaji (vile wanavyofikiria uzao unapaswa kufanana), huweka sheria za maonyesho ya mbwa, na mara nyingine programu za mafunzo (ambapo mbwa hufundishwa kufanya jambo fulani).

Mifano ya klabu za mbwa ni pamoja na Klabu ya Mbwa ya Marekani (American Kennel Club - AKC), Baraza la Taifa la Klabu ya Mbwa la Australia (Australian National Kennel Council), Klabu ya Mbwa ya Kanada (Canadian Kennel Club - CKC), na Klabu ya Mbwa ya Uingereza (The Kennel Club - United Kingdom).
Kuna aina nyingi za klabu za mbwa. Zinaweza kuwa “klabu za mbwa wa aina zote” (ambapo kuna orodha ya mbwa ambao wameamua kutambua), au klabu ya uzao moja ambayo hushughulikia uzao mmoja pekee.
Wakati mwingine, klabu ya mbwa hushughulikia aina moja ya mbwa tu.
Remove ads
Tazama pia
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads