Lugha ya kwanza

From Wikipedia, the free encyclopedia

Lugha ya kwanza
Remove ads

Lugha ya kwanza ni lugha ambayo mtu anaiongea kama lugha yake ya kwanza tangu utotoni[1], umri ambamo ni rahisi zaidi kuathiriwa na mazingira na hivyo pia kujifunza kusema kama watu wa kandokando [2] .

Thumb
Mnara kwa lugha mama (ana dili) huko Nakhchivan, Azerbaijan.
Thumb
Sikukuu ya lugha mama mjini Sydney, Australia, 19 Februari 2006

Pia lugha hiyo huitwa lugha mama (kwa Kiingereza "mother tongue") kwa vile watu wengi hujifunza lugha yao ya kwanza kutoka kwa mama mzazi. Lakini hiyo si lazima: mara nyingine mtoto halelewi na mama, au kama analelewa, anatumia muda mrefu zaidi na watoto wenzake (hasa shuleni), hivyo anazoea lugha yao kuliko ile ya nyumbani, hata kama ni tofauti kabisa.

Kwa sababu hiyohiyo wapo watu wenye lugha mama zaidi ya moja[3].

Tarehe 17 Novemba 1999, UNESCO iliteua tarehe 21 Februari ya kila mwaka kuwa Siku ya Kimataifa ya Lughamama.

Remove ads

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads