Ngeli

ngeli From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Ngeli ni makundi ya kisarufi ya majina katika lugha ya Kiswahili na lugha nyingine za Kibantu.

Kwa maneno mengine, ngeli za nomino ni utaratibu unaotumika kuweka nomino katika matabaka au makundi yanayofanana.

Mifano
  1. Maji yakimwagika hayazoleki.
  2. Mayai yaliyooza yananuka sana.
  3. Yai lililooza linanuka sana.
  4. Maji lililomwagika hayazoleki.

Katika mifano hiyo juu tunaona kwamba sentensi a, b na c ziko sahihi wakati sentensi d si sahihi, kwa sababu imekiuka upatanisho wa kisarufi. Kwa maana hiyo sentensi ‘a’ ipo katika ngeli ya YA-YA na sentensi b na c zipo katika ngeli ya LI-YA. Sentensi si sahihi kwa sababu nomino maji haina umoja, kwa hiyo haiwezi kuingia katika ngeli ya LI-YA. Kwa msingi huo ngeli za nomino huzingatia sana upatanisho wa kisarufi.

Kwa ujumla, ngeli za Kiswahili huainishwa kulingana na viambishi mbalimbali ambavyo nomino tofauti huchukua katika umoja na wingi.

Remove ads

Mipangilio na idadi yake

Jedwali lifuatalo linaonesha ngeli za nomino kwa misingi ya upatanisho wa kisarufi.

Maelezo zaidi Ufafanuzi, Mifano ...
Remove ads

Matumizi ya ngeli

Hapa tunaona dhima ya matumizi yake.

  • Hutumika kupanga majina ya lugha katika makundi yaliyoshikamana na kutofungamana kutokana na kigezo muhimu.
  • Hutumika kutambulisha maumbo ya umoja na wingi katika majina na vivumishi.
  • Hutumika katika upatanishi wa kisarufi katika sentensi.
  • Hutumika katika kuonyesha uhusiano uliopo baina ya lugha za Kiswahili na lugha nyingine.

Dhana ya O-rejeshi

O-rejeshi ni kiambishi kinachotumiwa kurejelea nomino ambayo huwa imetajwa kabla ya kitenzi chenyewe kutajwa. Viambishi hivyo ndivyo vinavyosababisha utegemezi katika sentensi.

Dhima kuu ya muundo wa O-rejeshi

Hutumika kama kirejeshi. Kwa mfano:

  • Mtu aliyepigwa jana na wananchi ni mfanyabiashara wa Mwanza.
  • O-rejeshi hudokeza mahali. Kwa mfano; rudisha ulipokitoa!
  • O- rejeshi hudokeza wakati. Kwa mfano; Alipokuja alinikuta nimelala.
  • Vilevile hutumika kama kiunganishi. Kwa mfano; Alikuja. Nilikuwa nimelala (alipokuja alinikuta nimelala)
  • Hudokeza namna. Mfano; Kila mtu anashangaa alivyoumia.

Kwa jumla, ngeli za Kiswahili huainishwa kulingana na viambishi mbalimbali ambavyo nomino tofauti huchukua katika umoja na wingi.

Remove ads

Tazama pia

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads