Wakarmeli Peku
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Wakarmeli Peku (kwa Kilatini Ordo Fratrum Discalceatorum B. Mariae V. de Monte Carmelo, kifupi O.C.D.) ni watawa wa Kanisa Katoliki wanaofuata urekebisho wa shirika la Wakarmeli ulioanzishwa na Teresa wa Yesu katika karne ya 16 huko Hispania. Upande wa wanaume alisaidiwa na Yohane wa Msalaba.

Mbali ya waanzilishi hao wawili, shirika lilizaa mwalimu wa Kanisa mwingine, Teresa wa Mtoto Yesu katika karne ya 19.
Kwa jumla hao watatu wanatazamwa kuwa viongozi bora kuhusu kuzama katika sala na maisha ya kiroho kwa jumla.
Pia shirika lilizaa watakatifu na wenye heri wengi.
Mwishoni mwa mwaka 2022 shirika lilikuwa na nyumba 572 zenye watawa 3,978, (kati yao mapadri 2,897).[1]
Remove ads
Picha
- Wakarmeli Peku walivyochorwa na Wenzel Hollar, mwaka 1650 hivi.
- Benedict Buns, mwaka 1716 hivi.
- Nembo ya shirika katika Manuscrito de Sanlúcar ya Yohane wa Msalaba.
- Konventi ya Segovia.
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads