Nusukipenyo ya Jua

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Nusukipenyo ya Jua (ing. solar radius) ni nusu ya kipenyo cha Jua letu na hivyo sawa na umbali wa kilomita 696.342 au mara 109 nusukipenyo cha Dunia[1].

Umbali huu hutumiwa kama kizio katika sayansi ya astronomia kwa kutaja ukubwa wa magimba kwenye anga-nje hasa nyota.

Mfano wa matumizi yake ni mfumo wa Dunia na Mwezi: umbali kati ya Dunia na Mwezi ni takriban kilomita 384.400 au asilimia 55 za nusukipenyo ya Jua. Kama Jua lingechukua nafasi ya Dunia njia ya obiti ya Mwezi ingekuwa ndani ya Jua lenyewe.

Kipenyo na nusukipenyo ya Jua hubadilika kidogo kufuatana na sehemu ya kukipima kwa sababu Jua si tufe kamili. Kwa sababu hiyo kuna ufafanuzi wa Umoja wa Kimataifa wa Astronomia wa kuhesabu nusukipenyo ya Jua kuwa na mita 6.957×108 au kilomita 695.700 [2].

Alama yake ni R ambapo "R" inamaanisha "radius" na ☉ ni ishara ya Jua.

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads