Slovakia

From Wikipedia, the free encyclopedia

Slovakia
Remove ads

Slovakia (Kwa Kislovakia Slovenská republika), rasmi kama Jamhuri ya Slovakia, ni nchi isiyo na pwani katika Ulaya ya Kati, inayopakana na Polandi kaskazini, Ukraini mashariki, Hungaria kusini, Austria kusini-magharibi, na Jamhuri ya Czech magharibi. Ina idadi ya watu takriban milioni 5.4, ikiwa ya 117 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Bratislava. Slovakia imegawanyika katika mikoa 8 (kraj). Inajulikana kwa milima yake ya Tatras, majumba ya kihistoria, na mchanganyiko wake wa utamaduni wa Kislavic na Kati ya Ulaya.

Ukweli wa haraka


Thumb

Slovakia imekuwa nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu tarehe 1 Mei 2004.

Miji muhimu baada ya Bratislava ni Košice, Banská Bystrica, Žilina, Trenčín, Nitra, Prešov na Trnava.

Wakazi walio wengi wanasema Kislovakia, ambacho ni kati ya lugha za Kislavoni, lakini kieneo kuna pia wasemaji wa Kihungaria, Kibelarus na Kiukraine.

Upande wa dini, 65.8% ni Wakatoliki, 8.9% Waprotestanti. 13.4% wanajitambulisha kama Wakanamungu.

Remove ads

Historia

Kwa sehemu kubwa ya historia yake hadi mwaka 1918 Slovakia ilikuwa chini ya watawala wa Habsburg waliokuwa wafalme na makaisari wa Austria.

Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia Slovakia ilipata uhuru pamoja na Ucheki katika nchi ya Chekoslovakia.

Mwaka 1993 Ucheki na Slovakia ziliachana kwa amani na kuwa kila moja nchi ya pekee.

Viungo vya nje


Maelezo zaidi Nchi za Umoja wa Ulaya ...
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Slovakia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads