Theodori wa Canterbury

From Wikipedia, the free encyclopedia

Theodori wa Canterbury
Remove ads

Theodori wa Canterbury (Tarso, Kilikia, leo nchini Uturuki, 602 - Canterbury, Kent, Uingereza, 19 Septemba 690) alikuwa askofu wa jimbo kuu hilo kwa miaka 22, akiliongoza kwa nguvu ingawa mzee tayari.

Thumb
Mt. Theodori.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Maisha

Msomi tayari, baada ya Waarabu kuteka mji wake (637) alihamia Konstantinopoli kuendelea na masomo mbalimbali, halafu mwaka 660 alihamia Roma katika monasteri ya Ukristo wa mashariki.

Papa Vitalian alimteua kuwa askofu mkuu wa Canterbury, akamweka wakfu tarehe 26 Machi 668.

Alirekebisha Kanisa la Uingereza lifuate mapokeo ya Roma akaanzisha shule ya Canterbury pamoja na Adriani wa Canterbury.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads