Andorra
From Wikipedia, the free encyclopedia
Utemi wa Andorra (Kikatalani: Principat d'Andorra, Kifaransa: Principauté d'Andorre) ni nchi ndogo katika Ulaya ya kusini magharibi.
Ukweli wa haraka
Andorra |
---|
Funga
Katiba yake ni ya utemi lakini kuna watemi wawili, nao wako nje ya nchi. Mmoja ni rais wa Ufaransa na mwingine ni askofu wa Urgell katika Hispania.
Andorra ni nchi mwanachama ya Baraza la Ulaya lakini si ya Umoja wa Ulaya. Hivyo si sehemu ya eneo la kodi za pamoja la Ulaya. Hali hii inavuta watalii kwa sababu bidhaa nyingi zinapatikana bila kodi kwa bei nafuu kuliko Hispania au Ufaransa; kodi ya ongezeko la thamani (VAT) iko kwenye 4% pekee.
Andorra inatumia pesa ya Euro bila kushiriki katika mkataba wa Euro.
Siku hizi imekuwa nchi tajiri kutokana na utalii.