Gregori Mletamwanga
From Wikipedia, the free encyclopedia
Gregori Mletamwanga (kwa Kiarmenia Գրիգոր Լուսաւորիչ, Grigor Lusavorich, 257 hivi - 331 hivi) ndiye mwanzilishi na kiongozi wa kwanza wa Kanisa la Kitume la Armenia kwa kuongoa nchi nzima ya Armenia kutoka Upagani kuingia Ukristo mwaka 301. Hivyo Armenia ikawa taifa la kwanza kufanya dini hiyo kuwa dini yake rasmi.
Tangu kale anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu.
Sikukuu yake inaadhimishwa na Waarmenia tarehe 9 Juni, lakini na Wakristo wengine tarehe 30 Septemba[1].