Kukausha kwa moshi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kukausha kwa moshi ni mbinu ya kutunza vyakula ili visiharibike haraka. Kwa njia hiyo chakula hupokea pia ladha maalumu.
Hutumiwa hasa kwa nyama na samaki, mara chache pia kwa mboga ya majani lakini hapo zaidi ni shauri la ladha.
Kama hatua ya kwanza nyama au samaki hutiwa chumvi. Chumvi huondoa sehemu ya maji ndani yake na kuzuia bakteria wengi ambao wanaweza kusababisha uharibifu.
Katika hatua ya pili nyama iliyoandaliwa vile huweka juu ya moshi wa moto. Hapo kiwango cha maji hupungua zaidi. Kemikali katika moshi wa moto wa mbao huzuia tena bakteria. Uso wa kile kinachotiwa moshi hukauka zaidi na kuwa mgumu kiasi na hivyo kuna kizuizi cha ziada dhidi ya kuingia kwa bakteria na wadudu[1].