Abdulrazak Gurnah
From Wikipedia, the free encyclopedia
Abdulrazak Gurnah Al Kindi (amezaliwa Zanzibar, 20 Desemba 1948[1] ) ni mwandishi mwenye asili ya Zanzibar aliyeishi nchini Uingereza tangu mwaka 1968. Huko anafundisha katika Chuo Kikuu cha Kent tangu mwaka 1982.
Tangu mwaka wa 1987 alitolea riwaya kadhaa kwa lugha ya Kiingereza. Mwaka 2021 alipewa tuzo ya Nobel ya Fasihi[2][3].