Ambrosi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Aureli Ambrosi (Trier, leo nchini Ujerumani, 340 hivi - Milano, Italia, 4 Aprili 397), alikuwa askofu wa Milano kuanzia mwaka 374 hadi kifo chake.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/9/9a/AmbroseOfMilan.jpg/220px-AmbroseOfMilan.jpg)
Ndiye aliyemuongoa na kumbatiza Agostino wa Hippo
Kati ya mambo ya pekee aliyoacha ni urithi wa tenzi na liturujia ya pekee inayoendelea kutumika Milano na sehemu nyingine kadhaa za Italia kaskazini na Uswisi ("liturujia ya Kiambrosi").
Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu na babu wa Kanisa.
Mwaka 1298 Papa Bonifasi VIII alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa.