Mwalimu wa Kanisa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mwalimu wa Kanisa ni jina la heshima ambalo kwa nadra Kanisa Katoliki linampa mtakatifu ambaye katika maisha, mafundisho na maandishi yake alionyesha na kueneza mwanga wa pekee katika masuala ya imani, maadili na maisha ya kiroho.
Maelezo zaidi Imani, Muundo ...
Funga
“Tamko la kwamba mtakatifu fulani ni Mwalimu wa Kanisa lote linategemea utambuzi wa karama maalumu ya hekima ambayo alijaliwa na Roho Mtakatifu kwa faida ya Kanisa ikabainishwa na athari njema ya mafundisho yake katika Taifa la Mungu” (Papa Benedikto XVI, Barua ya Kitume ya tarehe 7 Oktoba 2012).