Basil wa Caesarea
From Wikipedia, the free encyclopedia
Basili wa Kaisarea (Kaisarea wa Kapadokia, leo Kayseri, nchini Uturuki, takriban 329 – Kaisarea wa Kapadokia, 1 Januari, 379) alikuwa mmonaki, halafu askofu wa mji huo (mkoa wa Kapadokia, leo nchini Uturuki).
Ni mmojawapo kati ya Mababu wa Kanisa muhimu zaidi. Ndiyo sababu anaitwa Basili Mkuu (kwa Kigiriki Βασίλειος ο Μέγας).
Kwa jinsi alivyomkazia macho Kristo na kupenda watu, alianza kuheshimiwa kama mtakatifu punde baada ya kifo chake, na mwaka 1568 Papa Pius V alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa.