Bundesliga
From Wikipedia, the free encyclopedia
Bundesliga ni jina linalotumika katika michezo mbalimbali huko Ujerumani na Austria. Mpira wa miguu ni mchezo mashuhuri sana katika nchi hizo mbili. Na ndiyo maana mchezo wa mpira wa miguu unajulikana sana katika nchi hizo kwa jina la Bundesliga.
Timu za mpira zinaingia katika Bundesliga kwa kuwa washindi katika moja kati ya ligi ndogo za nchini humo. Timu itakayoongoza katika msimu wa mashindano hayo inaitwa Meister. Meister ni neno la Kijerumani lenye maana ya bingwa au mshindi. Kisheria, msimu wa michezo ya mpira huwa na kawaida ya kuanza Juni katika mwaka uliopo hadi Juni mwaka unaofuatia. Timu itakayoongoza itategemea na ushindi au pointi walizozipata wakati wa msimu huo. Msimu huo umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili.
Vilabu hamsini na sita vimefanikiwa kushiriki katika ligi hiyo ya Bundesliga tangu kuanzishwa kwake. Bayern Munich imeshinda kombe hilo mara 31. Hata hivyo Bundesliga imekua na mabingwa wengine kama Borussia Dortmund, Hamburger SV, Werder Bremen, Borussia Mönchengladbach, na VfB Stuttgart maarufu zaidi miongoni mwao. Bundesliga ni moja ya ligi kubwa kitaifa zilizoshika nafasi ya nne barani Ulaya kulingana na kiwango cha ubora katika ligi ya UEFA kwa msimu wa 2021-2022. Wachezaji wake wamekusanya tuzo tisa za Ballon d'Or, tuzo mbili za mchezaji bora wa FIFA, Viatu vinne vya dhahabu Ulaya, na tuzo tatu za mchezaji wa mwaka wa UEFA kwa wanaume ikiwa ni pamoja na Mchezaji bora wa Mwaka katika mashindano ya UEFA klabu.[1][2]
Bundesliga ni ligi ya soka namba moja duniani kwa wastani wa mashabiki 45,134 kwa kila mchezo wakati wa msimu wa 2011-12 Bundesliga hutangazwa kwenye televisheni katika nchi zaidi ya 200. Bundesliga ilianzishwa mwaka 1962 katika mji wa Dortmund na msimu wa kwanza ulianza mwaka 1963-64. muundo na shirika la Bundesliga, pamoja na ligi nyingine za soka za Ujerumani, zimefanyika mabadiliko ya mara kwa mara. Bundesliga ilianzishwa na Ujerumani Fußball-Bund. Shirikisho la Soka la Ujerumani), lakini kwa sasa inaendeshwa na Deutsche Fußball Liga.