Viluwiri ni ndege wa jenasi mbalimbali za familia ya Rallidae. Spishi za jenasi Rallus zinaitwa kibilinzi pia. Viluwiri wa Afrika wana rangi zilizofifia na hawaoneki rahisi wotoni, lakini husikika mara zaidi. Wana domo refu, miguu myembamba na vidole virefu. Spishi nyingi zaidi zinatokea karibu na maji, mabwawani au nyikani majimaji ambapo hula wadudu na wanyama wadogo wa maji na wa matope. Kwa kawaida tago lao limefanyika kwa mimea ya maji kwa umbo wa bakuli mahali pakavu katika bwawa na huyataga mayai 2-12.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Kiluwiri |
Kiluwiri mweusi |
Uainishaji wa kisayansi |
Himaya: |
Animalia (Wanyama)
|
Faila: |
Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
|
Nusufaila: |
Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
|
Ngeli: |
Aves (Ndege)
|
Oda: |
Gruiformes (Ndege kama korongo)
|
Familia: |
Rallidae (Ndege walio na mnasaba na viluwiri) Rafinesque, 1815 |
|
Ngazi za chini |
Jenasi 29:
- Aenigmatolimnas Peters, 1932
- Amaurolimnas Sharpe, 1893
- Amaurornis Reichenbach, 1853
- Anurolimnas Sharpe, 1893
- Aramides Pucheran, 1845
- Aramidopsis Sharpe, 1893
- Atlantisia Lowe, 1923
- Coturnicops Gray, 1855
- Crecopsis Sharpe, 1893
- Crex Bechstein, 1803
- Cyanolimnas Barbour & Peters, 1927
- Dryolimnas Sharpe, 1893
- Eulabeornis Gould, 1844
- Gallirallus Lafresnaye, 1841
- Gymnocrex Salvadori, 1875
- Habroptila Gray, 1860
- Himantornis Hartlaub, 1855
- Laterallus Gray, 1855
- Lewinia Gray, 1855
- Megacrex Albertis & Salvadori, 1879
- Micropygia Bonaparte, 1856
- Neocrex Sclater & Salvin, 1869
- Nesoclopeus Peters, 1932
- Pardirallus Bonaparte, 1856
- Porzana Vieillot, 1816
- Rallina Gray, 1846
- Rallus Linnaeus, 1758
- Rougetius Bonaparte, 1856
|
Funga