Klemens wa Aleksandria
From Wikipedia, the free encyclopedia
Titus Flavius Clemens (anayejulikana zaidi kama Klemens wa Aleksandria; kwa Kigiriki: Κλήμης Αλεξανδρεύς, Klemes Alexandreus; Athens, 150 hivi; Aleksandria, 215 hivi) alikuwa mwanafalsafa na mwanateolojia wa Ukristo katika mji wa Aleksandria (Misri) mwanzoni mwa karne ya 3[1].
Huhesabiwa kati ya walimu muhimu wa Kanisa la kwanza.
Anaheshimiwa na Waorthodoksi wa Mashariki, Waanglikana na wengineo kama mtakatifu.