Mabomu ya Hiroshima na Nagasaki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mabomu ya Hiroshima na Nagasaki yalikuwa silaha za nyuklia za kwanza katika historia ya binadamu. Zilirushwa na jeshi la Marekani kwenye Agosti wa mwaka 1945 juu ya miji ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japani na kusababisha mara moja vifo vya watu 100,000 hivi, waliofuatwa na 130,00 za ziada waliokufa kutokana na majeraha na mnururisho katika mwaka 1945. Milipuko, pamoja na mashambulio kutoka Urusi, ilifanya serikali ya Japani kusalimisha amri na hivyo kuleta mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia[1].