Matengenezo ya Kiprotestanti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Matengenezo ya Kiprotestanti ni muda wa mifululizo ya matukio ambayo yalitokea katika karne ya 16 katika Ukristo, hasa miaka 1517-1555, yaani kuanzia uenezi wa hoja 95 za Martin Luther hadi amani ya Augsburg.
Kati yake chanzo, yaani mabishano ya Kikanisa yaliyosababishwa na teolojia ya Luther, yalichanganyikana mapema na siasa, uchumi na utamaduni, kutokana na hali halisi ya wakati huo, mbali kuliko mwenyewe alivyofikiri.