Muujiza
From Wikipedia, the free encyclopedia
Muujiza ni tukio lisiloelezeka kisayansi kufuatana na sheria za maumbile.[1]
Matukio hayo yanaweza kufikiriwa yamesababishwa ama na Mungu au miungu, hata kupitia mtu wa dini, ama na nguvu nyingine zinazohusiana na ushirikina.
Hayo ni tofauti kabisa na matukio ambayo yanapatikana kwa nadra lakini yanaweza kuelezwa kisayansi ambayo watu wengine wakiyashangaa na kuyafurahia wanayaita miujiza.