Papa Gregori XIII
From Wikipedia, the free encyclopedia
Papa Gregori XIII (Bologna, Italia, 7 Januari 1502; Roma, 10 Aprili 1585) alikuwa Papa wa Kanisa Katoliki kuanzia tarehe 13/25 Mei 1572 hadi kifo chake[1]. Alitokea Bologna, Italia[2].
Alimfuata Papa Pius V akafuatwa na Papa Sixtus V.
Anakumbukwa hasa kwa matengenezo ya kalenda iliyokuja kujulikana kama "kalenda ya Gregori" ikawa kalenda ya kimataifa kote duniani hadi leo.