Paul Rusesabagina
From Wikipedia, the free encyclopedia
Paul Rusesabagina (alizaliwa Murama, Gitarama, Rwanda, 15 Juni 1954) ni raia wa Rwanda aliyekuwa meneja wa Hotel des Mille Collines mjini Kigali. Wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda aliwalinda Wahutu na Watutsi waliokimbilia hoteli yake na hivyo kuokoa watu 1268 dhidi ya wanamgambo wa Interahamwe.
Kazi wa Paul Rusesabagina ilikuwa msingi wa filamu ya “Hotel Rwanda” iliyofanyika mwaka 2004. Rusesabagina alionyeshwa na Don Cheadle, mwigizaji wa Marekani.
Anaishi katika mji wa Brussels katika nchi ya Ubelgiji na mji wa San Antonio katika jimbo la Texas nchi ya Marekani. Yeye ana nyumba katika miji miwili.
Rusesabagina alianza “Hotel Rwanda Rusesabagina Foundation” kupigania haki za binadamu duniani.[1]