Paulina Visintainer
From Wikipedia, the free encyclopedia
Paulina Visintainer (Vigolo Vattaro[1], leo nchini Italia, 16 Desemba 1865 - Ipiranga, Brazil, 8 Julai 1942) alikuwa bikira wa Italia kaskazini ambaye alihamia Brazil katika ujana wake akaanzisha huko shirika la Masista Wadogo wa Kukingiwa Dhambi ya Asili kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa na maskini.
Baada ya matatizo mengi, alitumikia shirika hilo kwa unyenyekevu mkubwa na sala ya kudumu[2]
Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwenye heri tarehe 18 Oktoba 1991, halafu mtakatifu tarehe 19 Mei 2002.